Umesikia alichokisema dada yake na Cristiano Ronaldo kuhusu wahuni walioipaka rangi sanamu ya kaka yake na kuandika jina la Messi?

Sanamu ya Cristiano Ronaldo iliyoharibiwa kwa rangi.
Baada ya Lionel Messi kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa dunia (Balon d`or) kwa mara ya tano pale jijini Zurich Uswizi na Cristiano Ronaldo akishika nafasi ya pili, kule kijijini kwa kina Cristiano Ronaldo kwenye kisiwa cha Madeira kulizuka watu wanaosadikika kuwa ni mashabiki wa mchezaji Lionel Messi na wengine wakisema kuwa sio mashabiki wa Lionel Messi bali ni wahuni wasiomkubali Cristiano Ronaldo na waliipaka rangi mbalimbali huku wakiiandika jina la Lionel Messi na namba 10 mgongoni ile sanamu ya Cristiano Ronaldo iliyowekwa mwaka jana majira kama haya baada ya kushinda tuzo yake ya tatu ya Balon d`or kwa mwaka 2014.
Katia Aveiro, dada yake na Cristiano Ronaldo.
Baada ya tukio hilo kutokea dada yake na Cristiano Ronaldo aitwaye Katia Aveiro alisema anasikitishwa sana na kitendo hicho na kusema kwamba roho imemuuma sana kwakuwa kaka yake hastahili utovu huo wa nidhamu kwa heshima aliyowaletea katika kisiwa hicho akipendacho cha Madeira na kusisitiza kuwa wahuni hao wanafaa kwenda kuishi nchini Syria maana wanafaa kukaa sehemu yenye vita kama hiyo huku akiomba msamaha kwa wote wanaoishi nchini Syria akisema kuwa wapo ambao hawastahili kuishi kwenye mazingira hayo ila anaomba Mungu awaepushe na adha hiyo ya vita.
Share on Google Plus

About Kings

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment