Manchester United yamwania beki kisiki wa Brazil.
-Taarifa zinaeleza kuwa klabu ya Manchester United imevutiwa na huduma ya beki wa kati wa timu ya taifa ya Brazil na klabu yake ya Atletico Madrid Joao Miranda. Miranda ameichezea timu yake ya taifa mara 27 na sasa yupo klabu ya Inter Milan kwa mkopo wa miaka miwili akitokea Atletico Madrid. Manchester United wanataka kumchukua beki huyo pindi atakapomaliza mkopo wake ili kuimarisha safu ya ulinzi ya timu hiyo ambayo imeonekana kupwaya mara kwa mara. Miaka miwili ya mkopo wa Miranda itaisha mwisho wa msimu huu.
0 comments:
Post a Comment