Liverpool na Arsenal zatoa heshima kwa Ronaldo.

 Uwanja wa Anfield unaotumiwa na majogoo wa jiji la Liverpool jumanne iliyopita ulisimama kutoa heshima kwa mshambuliaji wa mashetani wekundu Manchester United Cristiano Ronaldo baada ya kuondokewa na mtoto wake wa kiume. Pia katika mchezo wa Jumamosi uwanja wa Emirates unaotumiwa na washika bunduki wa London klabu ya Arsenal ulitoa heshima kwa mchezaji huyu bora wa dunia mara tano. Hili ni tukio la kihistoria na kiungwana kwa wapenda soka wote duniani na limepongezwa na wapenzi wengi wa soka duniani.



Share on Google Plus

About Kings

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment